Posts

Showing posts from March, 2021

SERIKALI KUENDELEA KUZIPATIA UFUMBUZI CHANGAMOTO ZA MUUNGANO

Image
    Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria wakiwa wamesimama kwa dakika moja kabla ya kuanza kwa kikao cha Kamati ikiwa ni ishara ya kumkumbuka aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano na Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Joseph Magulifuli. Kamati hiyo imekutana hii leo Machi 28, 2021 katika Ukumbi wa Msekwa jijini Dodoma kujadili  taarifa ya Utekelezaji wa Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa fedha 2020/2021 na Makadirio ya Mapato na Matumizi  kwa mwaka wa fedha 2021/2022. Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Ummy Mwalimu  (kushoto) akiwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa fedha 2020/2021 na Makadirio ya Mapato na Matumizi  kwa mwaka wa fedha 2021/2022 mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria hii leo Machi 28, 2021 katika Ukumbi wa Msekwa jijini Dodoma. Meza kuu ni Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Mohamed Mchengerwa (katikati) Makamu Mwenyekiti Mhe. Najma Giga na Katibu wa Kamati ...

RAIS SAMIA AANZA NA WAANDISHI WA HABARI

Image
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akila kiapo cha uaminifu   Na John Mapepele, Dodoma Tanzania imeandika historia ya kuwa na Rais mwanamke wa kwanza kwenye nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki ambapo Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan ameapishwa rasmi tarehe 19 Machi, 2021 kushika wadhifa huo kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Tanzania Hayati Mhe, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kilichotokea tarehe 17 Machi, 2021.   Kwa Mujibu wa ibara ya 37(5) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano, endapo kiti cha Rais kitakuwa wazi kutokana na Rais kufariki dunia, kijiuzulu, kupoteza sifa za uchaguzi au kutomudu kazi zake kutokana namaradhi ya mwili au  kushindwa  kutekeleza kazi za rais, basi  Makamu wa Rais ataapishwa  na atakuwa Rais kwa muda  uliobaki katika kipindi cha miaka mitano.   Mara baada ya kula kiapo Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan akiwa na majon...